Ads (728x90)



Mambo muhimu ya kuyafahamu
1.    Kware aina ya Japanese ni kware anaefugwa ndani ya uzio na katika banda la wavu.
2.    Si vizuri aishi na kinyesi chake.
3.    Kware aina ya japanese ni tofauti na kware wa porini anaepatikana Tanzania.

Chakula.

1.    Kware anakula chakula chochote anachoweza kula kuku ikiwemo chakula cha broiler. Kama utaamua kuwapa chakula cha broiler unawapa “starter” kware wenye umri kuanzia siku moja hadi wiki ya tatu  baada ya hapo unawapa Falcon au hill.

2.    Ukiweza kuwatengenezea chakula chako mwenye kutumia pumba nk. Ni vizuri zaidi kwa mayai yenye lishe 100%

3.    Kware 100 wenye umri wa mwezi hutumia kiroba cha kilo 20 kwa wiki 3.

4.    Kware hawamalizi chakula kama kuku.

5.    Pia kware hupewa majani kama mchicha nk.



Magonjwa:
1.    Kware hawa hawasumbuliwi na magonjwa bali hudonoana tu wenyewe endapo watawekwa wengi katika sehemu ndogo. Hivyo ni lazima uwe na majani ya aroevela karibu kwa ajili ya kuwapaka maji yake pale wanapoumia.

ZINGATIA:

Wanapokosa madini ya kutosha kwenye chakula huweza kupata madhara yafuatayo:-
1.    Kuharisha
2.    Kunyonyoka manyoya
3.    Kupunguza kasi ya kutaga mayai.


Post a Comment

  1. habari za kazi, samahani nimevutiwa sana na ufugaji wa kware. sasa kwa hapa Tanzania naweza kuwapata wapi?

    ReplyDelete